Rais
Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akifunga semina ya Mawaziri na Makatibu Wakuu ili
kupanga mikakati ya utekelezaji wa mfumo mpya kusimamia utekelezaji,
ufuatiliaji tathmini na miradi ya maendeleo uliofanyika katika ukumbi wa St
Gaspar mjini Dodoma. Mfumo huo unaanza kutekelezwa kwa kutumia uzoefu wa
Performance Management and Delivery Unit (PEMANDU) ya Malaysia. Mfumo huu
utajumuisha uanzishwaji wa taasisi ya President's Delivery Bureau (PDB) ambayo
itafanya kazi kwa karibu na Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango. Katika mfumo huu,
uchambuzi wa kina wa kimaabara (labs) utafanyika ili kuandaa programu za
utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Awamu ya kwanza ya labs ilizinduliwa rasmi
na Rais Kikwete tarehe 22 Februari, 2013 na kukamilika Aprili, 2013. Maeneo ya
awamu ya Kwanza wa kimaabara ( labs) yanahusisha elimu, kilimo, nishati,
mapato, maji, miundombinu na uchukuzi.
Rais Dk. Jakaya M. Kikwete, na Makamu , Rais Dk.Mohamed
Gharib Bilali na Katibu Mkuu Kiongozi Ombeni Sefue wakiweka sahihi kama wadhamini wa waraka katika utekelezaji wa
mfumo mpya wa kusimamia utekelezaji, ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya
maendeleo uliokabidhiwa kwa wizara hizo sita katika semina elekezi kwa mawaziri
na makatibu wakuu iliyofanyika katika ukumbi wa St Gaspar mjini Dodoma.
Rais Dk. Jakaya M. Kikwete akiongea wakati wa semina kwa Mawaziri
na Makatibu Wakuu kujadili mikakati ya utekelezaji WA WA mfumo mpya kusimamia
utekelezaji, na ufuatiliaji tathmini ya miradi ya maendeleo katika ukumbi wa St
Gaspar mjini Dodoma.
Mawaziri
wa Fedha, Kilimo, Uchukuzi, Maji, Nishati na na Madini Elimu wakiweka saini
waraka wa utekelezaji wa mfumo mpya kusimamia utekelezaji , ufuatiliaji na
tathmini ya miradi ya maendeleo uliokabidhiwa kwa wizara sita hizo sita baada
ya semina elekezi kwa mawaziri na makatibu wakuu iliyofanyika ukumbi wa St
Gaspar mjini Dodoma.
Rais Dk. Jakaya M. Kikwete, na Makamu , Rais Dk.Mohamed
Gharib Bilali na Katibu Mkuu Kiongozi Ndg. Ombeni Sefue wakiwa na Mawaziri na Makatibu
Wakuu wakimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa Performance Management and Delivery
Unit (PEMANDU) wa Malaysia Dkt Idris Jala wakati wa kuujadili mfumo mpya wa
kusimamia utekelezaji, ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya maendeleo
uliokabidhiwa kwa wizara hizo sita katika semina elekezi kwa Mawaziri na Makatibu
Wakuu iliyofanyika ukumbi wa
St Gaspar mjini Dodoma.
St Gaspar mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki
ya Zamani ya NBC Ndg. Lawrence Mafuru
akitoa majumuisho ya uchambuzi wa kimaabara kwa kina (labs) mfumo mpya wa
kusimamia utekelezaji, ufuatiliaji tathmini na ya ya miradi maendeleo katika semina
elekezi kwa Mawaziri na Makatibu Wakuu
iliyofanyika ukumbi wa St Gaspar mjini
Dodoma. picha NA IKULU (MICHUZI)
No comments:
Post a Comment