Wednesday, July 17, 2013

Miradi miwili ya maendeleo wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma yote ikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.6imezinduliwa

Waziri Mkuu aweka jiwe la msingi na kuzindua miradi ya maendeleo Namtumbo


Waziri Mkuu Mizengo kayanza Pinda akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Hospital ya Wilaya ya Namtumbo

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikata utepe kuashiria uzinduzi wa machinjio ya kisasa katika mji mdogo wa Namtumbo akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma

 Baadhi ya Viongozi wakishangilia baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kukata utepe
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizundua  mitambo ya kuzalisha umeme katika mji mdogo wa Namtumbo akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma.

WAZIRI Mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda ameweka jiwe la msingi na kuzindua miradi miwili ya maendeleo wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma yote ikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.6.



Miradi hiyo iliyotembelewa kuwekwa jiwe la msingi na kuzinduliwa katika siku ya tatu ya ziara ya Waziri mkuu mkoani Ruvuma ni pamoja na hospitali ya wilaya ya Namtumbo iliyogharimu kiasi cha shilingi milioni 600 kwa ujenzi uliofikiwa na itakapokamilika itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 4.4 huku akizindua mradi wa machinjio ya kisasa ya mji wa Namtumbo ambayo yamegharimu kiasi cha shilingili milioni 148.

Katika hatua nyingine Waziri mkuu amewasha rasmi umeme wa jenereta katika mji huo wa Namtumbo ambao ujenzi wake umegharimu kiasi cha shilingi milioni 800 na kuwata wananchi wilayani humo kuitumia miradi hiyo yote kujiletea maendeleo ambayo yanapaswa kuibuliwa na wao wenyewe na serikali itatoa ushirikiano mkubwa katika kuifanya wilaya ya Nmtumbo kuwa ya kisasa zaidi.

Amesema kuwa kuwepo kwa umeme,hospitali na huduma nyingine za muhimu katika maendeleo kutawezekana kwa wananchi wenyewe kujituma katika kufanya kazi zaidi na hsa katika kilimo cha mazao mbali mbali kwa sababu ardhi ya wilaya ya Namtumbo inaruhusu kilimo cha mazao ya chakula na biashara.

Amesema kuwa maendeleo yoyote duniani huletwa na wananchi kwa kutumia ipasavyo fursa zilizopo katika maeneo yanayowazunguka hivyo amewataka wananchi wilayani Namtumbo na mkoani Ruvuma kwa ujumla kuzitumia fursa zilizopo kujiletea maendeleo na serikli itaunga mkono kwa dhati jitihada zozote za wananchi katika suala zima la kujiletea maendeleo.

Aidha amesema kuwa dhamira ya maendeleo huanza kwa mwananchi mmoja mmoja kwa kukubali kutumia fursa mbali mbali zilizopo katika eneo husika na siyo kwa kukaa na kulalamikia serikali kwa kuitaka iwaletee maendeleo bila wao kujishughulisha katika kuyatafuta maendeleo na amewataka wananchi kuitunza miradi yote ya maendeleo iliyopo kwa ajili ya manufaa yao na kizazi kijacho.

Waziri mkuu amewataka kutambua kuwa miradi hiyo yote imetumia gharama kubwa ambazozimetokana na kodi zao pamoja na wafadhili ambao nao wanatoa kama msaada kutoka kwenye kodi za wananchi wao hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuithamini miradi hiyo kwa ajili ya maendeleo yao.

Picha na habari kwa hisani ya demashonews.blogspot.com

No comments:

Post a Comment

 
Support : Katibu Mwenezi CCM (w) Arusha | Jasper Kishumbua | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali Blog - Arusha - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper Kishumbua
Proudly powered by Blogger