Saturday, February 16, 2013

NAPE; BUNGE KURUSHWA LIVE KUTAIMALIZA CHADEMA


Azoa vigogo kibao wa Chadema.
Awafananisha na nguruwe anayekula watoto wake mwenyewe.
Awakumbusha upinzani si kupinga kila kitu.
Asema wananchi wanakerwa na fujo zao bungeni.
Adai zitapunguza idadi ya wabunge wao bungeni.
Zitashusha hadhi yao kwa umma.
Asema walitumwa kutetea wananchi, si kufanya fujo.
Awaambia kazi ndo kwanza imeanza.
Adai miaka 20 inatosha kuwakomaza.
 

Juliana Shonza akihutubia wakazi wa Temeke juu ya maamuzi yake thabiti ya kujiunga na CCM

 

Mtela Mwampamba akiwaeleza wananchi wa Temeke mapungufu makubwa ya kidemokrasia yaliyopo kwenye vyama vya upinzani na hivyo kumfanya yeye binafsi kuchukua uamuzi wa kujiunga na CCM.

 

 
Saumu Kisena akionyesha kitambulisho chake , Saumu amejiunga rasmi CCM baada ya kugundua chama alichokuwepo kinahubiri haki nje wakati ndani hamna haki kabisa.

 

Katibu wa NEC ,Itikadi na Uenezi, akihutubia wananchi wa Wilaya ya Temeke na kuwahakikishia kuwa CCM itaisimamia serikali itekeleze ilani yake ya Uchaguzi kwa asilimia 100.

 

Mkuu wa Wilaya ya Temeke ,Ndugu Sophia Mjema akiwapungia wananchi wa Temeke wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Pile ,Temeke ,Mwisho.

 

Wananchi na Wapenzi wa CCM kutoka kata ya Kilakala,Yombo kama walivyojitambulisha ,walisema Nape ameongea mambo mengi ya msingi na kumtakia heri aendelee kufanya kazi nzuri.

 

Wasanii wa kikundi cha TMK wakitoa burudani kwenye uwanja wa nyumbani wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Pile, Temeke,tarehe 16/2/2013.

 

Baadhi ya wananchi wakionekana kuelewa vizuri maneno ya viongozi wao.

 

Kikundi cha Hamasa cha CCM,Temeke kikihamasisha kwa aina yake wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Pile,Temeke.


Ndg. Nape ameyasema hayo jana kwenye mkutano mkubwa wa hadhara kwenye viwanja vya mwembe yanga Temeke wakati akihutubia maelfu ya wanachi na mashabiki wa chama hicho kwenye mkutano huo.



Mkutano huo umeandaliwa na CCM mkoa wa Dar es salaam kwa lengo la kujibu mapigo ya Chadema waliofanya mkutano wao siku ya jumapili.



Nape alisema, " watani zangu acheni kujiliza kila siku, mnaishia kulialia tu.  Mmekuja mwembe yanga nikadhani mna jambo la maana,kumbe kulialia tu! Yaani miaka ishirini ya vyama vingi bado mnajiliza tu? Mtakua lini?"



Nape akawndelea kusema kuwa uteuzi wa kamati kuu ya CCM ni ishara kuwa kazi imeanza,hivyo kujiliza kwao hakuta irudisha nyuma CCM.

" Tumekamilisha uchaguzi na upangaji wa safu ndani ya chama. Safu hii ina kazi kubwa mbili, kwanza kusukuma utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ili kuboresha maisha ya watanzania na kazi ya pili ni kuhakikisha CCM inashinda kwa kishindo 2014 na 2015"! Alisisitiza Nape



Akasema Chadema wameshindwa kukomaa mpaka sasa hata baada ya miaka 20 ya mfumo wa vyama vingi kwasababu wana tabia ya nguruwe ya kula watoto wake yenyewe.

" hawa watani kinachowamaliza ni kuwa na tabia ya nguruwe, nguruwe akishazaa watoto, akishikwa njaa hula watoto wake mwenyewe, sasa wao kila kukicha wanakula watoto wao wenyewe watakomaa lini?"alihoji Nape.



Nape anasema kwasababu ya kutokomaa kwa upinzani nchini ndo maana wamejenga tabia ya kupinga kila kitu hata yale yenye manufaa kwa wananchi.

"Mtashangaa kuwa wenzetu hupinga kila kitu cha serikali mpaka bajeti ambazo pesa zikipitishwa ndio zinajenga miundo mbinu kama barabara, zinaleta madawa, zinaajiri waalimu, zinalipa mishahara na hata posho wanazolipwa zinatokana na bajeti ya serikali, kwasababu ya tabia ya nguruwe kula hata watoto wake ilimradi ana njaa, basi wao hupinga kila kitu" alisema Nape.



"Angalieni bunge la bajeti mwezi wa nne mpaka wa saba, mtagundua hakuna mpinzani atakubali bajeti ya serikali, ambayo pesa ikipitishwa inakwenda kwenye majimbo yao pia. Bajeti iliyopita ni mpinzani mmoja tu nadhani alikubali bajeti ipite." Alieleza Nape.



Aidha Nape alisema kwenye kikao cha NEC kilichomalizika mjini Dodoma hivi karibuni pamoja na mambo mengine walijadili changamoto kubwa ya ajira nchini hasa kwa vijana na kuahidi kuwa swala hilo atalizungumzia kwa kina kwenye mkutano wa hadhara utakaofanyika Goba leo jioni.

No comments:

Post a Comment

 
Support : Katibu Mwenezi CCM (w) Arusha | Jasper Kishumbua | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali Blog - Arusha - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper Kishumbua
Proudly powered by Blogger