Saturday, March 9, 2013

Wabunge wa Tanzania Bara na Viswani waula AICC


Kituo cha kimataifa cha mikutano AICC kilichopo jijini Arusha







Na Fidelis Butahe, Mwananchi



KWA UFUPI



Wabunge hao ni Faith Mtambo na Mary Chatanda (wote viti maalumu (CCM), Mbunge wa Nzega (CCM), Dk Hamis  Kigwangala na  Ali Mzee Ali ambaye ni mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.



Wabunge watatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mmoja wa Baraza la wawakilishi Zanzibar wameteuliwa kuwa wajumbe wa Bodi ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).



Wabunge hao ni Faith Mtambo na Mary Chatanda (wote viti maalumu (CCM), Mbunge wa Nzega (CCM), Dk Hamis  Kigwangala na  Ali Mzee Ali ambaye ni mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.



Katika orodha hiyo ya wajumbe wapya, pia yumo Wilson Masilingi ambaye alikuwa Mbunge wa Muleba Kusini  mpaka mwaka 2010, ambapo alishindwa katika kura za maoni ndani ya chama chake na mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Profesa Anna Tibaijuka ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.



Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inaeleza kuwa , Rais Jakaya Kikwete amemteua kwa kipindi cha pili, Balozi Christopher Liundi kuwa mwenyekiti wa Bodi hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu na kwamba uteuzi huo umeanza rasmi Machi 6,mwaka huu.



Liundi aliteuliwa kushika nafasi hiyo mwaka 2010, huku wajumbe wake wakati huo wakiwa ni Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu, Rose Lugembe, Shabani Mnubi, Nuru Milao, Joseph Chilambo, Wilfred Nyachia, Makumba Kimweri, Dk Aggrey Mlimuka na Issa Suleiman.



Wajumbe wengine wa bodi hiyo mpya ni Aggrey Mlimuka,  Dash-Hood Mndeme, Dk Ali Mndali na  Balozi mstaafu Abdi Mshangama.

No comments:

Post a Comment

 
Support : Katibu Mwenezi CCM (w) Arusha | Jasper Kishumbua | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali Blog - Arusha - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper Kishumbua
Proudly powered by Blogger