Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akilakiwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Iddi Mohammed baada ya kuwasilili jioni hii kwenye Ofisi ya CCM mkoa huo mjini Moshi.
Leo Nape anatarajiwa kufungua Semina ya Halmashauri Kuu ya Mkoa huo ya CCM na baadaye kuhutubia Mkutano mkubwa wa hadhara mjini Moshi
Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Steven Kazidi (wapili kushoto) akimtambulisha Mwenyekiti wa UVCCM mkoa huo, Frederick Mushi kwa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kwenye
Ofisi ya CCM Mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Moshi Mjini Elizabeth Minde.
Nape akitia saini kwenye kitabu cha wageni, katika Ofisi ya CCM Mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi jana jioni mara baada ya kuwasili. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Iddi Mohammed.
No comments:
Post a Comment