Thursday, April 4, 2013

WAZIRI MKUU ATEMBELEA MAJERUHI HOSPITALI YA MOUNT MERU NA KUWAPA POLE WAFIWA

Waziri Mkuu Mh. Pinda akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Arusha Ndg W.Soileli akifuatiwa na Katibu wa CCM Wilaya ya Arusha Ndg Sabuni (mwenye kofia) akifuatiwa na Katibu wa Uchumi CCM Ndg H.Sood aliyevaa suti.


Waziri Mkuu Mh Pinda akisalimiana na Katibu Mwenezi wa CCM Kata ya Kati Ndg Zamzam katika uwanja wa ndege wa Arusha mara baada ya kuwasili, kulia kwake ni Katibu wa UWT CCM Mkoa wa Arusha Ndg Stamili Bendego


Waziri Mkuu Mh. Pinda akimfariji mmoja wa majeruhi aliyekuwa amelazwa kwenye wadi katika Hospitali ya Mt. Meru


Waziri Mkuu Mh. Pinda akiwa ameongozana na Mbunge wa viti Maalumu UVCCM (CCM) Mh. Catherine Magige wakiwafariji wagonjwa katika Hospitali ya Mount Meru.

Waziri Mkuu akisaini daftari la maombolezo

DSCF8584

Majeneza 13 katika eneo la chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Mkoa Mt.Meru

DSCF8607

Waziri Mkuu Mh. Pinda akifariji wafiwa
DSCF8591

Mch. Kisiri Laizer akitoa neno la pole kwa wafiwa

DSCF8592

Wafiwa wakiwa katika nyuso za huzuni ambapo wengine walishindwa kuvumilia na kuangua vilio

DSCF8599

Mstahiki Meya wa jiji Mh.Gaudence Lyimo akitoa salamu za pole kwa wafiwa

DSCF8613
Mh.Pinda akizungumza na kijana ambaye alinusurika katika tukio hilo ambaye hali yake inaendelea vizuri baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini
DSCF8600
Mkuu wa Mkoa Magessa Mulongo akitoa salamu za rambirambi kwa wafiwa

DSCF8623
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangalia hali halisi ya eneo la uchimbaji moramu katika Kata ya Moshono Mkoani Arusha akiwa na viongozi mbalimbali wa serikali na vyama jana tarehe 2/4/2013 ambapo watu 13 walipoteza maisha papo hapo

DSCF8638
Kushoto - kulia : Naibu Waziri wa Madini,Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha (aliyejifunga mtandio) wakifuatilia kwa makini alichokuwa anaeleza Waziri Mkuu.

DSCF8627
Mabki ya mojawapo ya gari aina ya Scania lili;oangukiwa na kifusi cha moramu.
DSCF8630
Eneo la tukio.

DSCF8636
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele akiwa anaongea na wananchi katika eneo hilo

DSCF8618
Eneo la tukio baada ya kufanyiwa usafi.


 
 

Waziri Mkuu Mizengo Pinda alitangaza kuyafunga rasmi machimbo ya moramu eneo la Moshono, Arusha hadi Serikali itakapoweka utaratibu mzuri wa shughuli mbalimbali za uchimbaji katika eneo hilo ili kuepusha maafa mengine



Hatua hiyo ya Pinda imetokana na ajali ya watu 13 waliopoteza maisha baada ya kufukiwa na kifusi juzi, wakati wengine wawili walijeruhiwa kwenye ajali hiyo iliyochangiwa kwa kiasi kikubwa na mvua zinazonyesha jijini Arusha.



Pinda alitoa agizo hilo alipotembelea eneo hilo pamoja na kuwajulia hali majeruhi wawili waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mt Meru.


Majeruhi mmojawapo aliruhusiwa kutoka hospitalini hapo baada ya kuondoka Waziri Mkuu.

Baada ya kuwasili Arusha jana saa 7.30 mchana, Pinda alikwenda moja kwa moja katika Hospitali ya Mt Meru kuwatembelea majeruhi hao.


Wakati wa ziara yake alishuhudia majeneza 13 yaliyokuwa na miili ya watu waliofariki kwenye tukio hilo ambayo imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti.


Akizungumza mara baada ya kutembelea eneo hilo Pinda alitoa salamu za pole kwa waathirika kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete huku akilishukuru Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na wananchi waliojitokeza kuokoa maisha ya watu katika tukio hilo. Alisema Serikali imeyafunga machimbo hayo, huku akisisitiza kuwa Serikali kamwe haiwezi kuruhusu uchimbaji wa namna hiyo.


“Tutafunga kwa muda kama tulivyofanya Mugusu ili tujipange vizuri na tupate nafasi ya kusaidiana, hatuwezi kuruhusu uchimbaji wa namna hii halafu kesho na keshokutwa tukaonekana wapuuzi,” alisema Pinda.

Waziri Mkuu pia alimwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo kushirikiana na JWTZ kuimarisha ulinzi mkali katika eneo hilo ili watu wasiweze kujipenyeza na kufanya uchimbaji nyakati za usiku.


“Mkuu wa Mkoa ashirikiane na jeshi kuimarisha ulinzi hapa najua ni gharama kwa Serikali lakini ni nafuu kwetu pia,”alisisitiza Pinda.



MASELE ALONGA.......


Naye Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele aliwatupia lawama baadhi ya viongozi wa Serikali na Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa tabia ya kuendeleza kuchukua mapato katika uchimbaji wa eneo hilo badala ya kuangalia usalama



Aliwataka viongozi wa jiji hilo kuacha tabia hiyo kwa kuwa ikiendelea kuna uwezekano mkubwa wa kuwapoteza wapiga kura ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa


"Viongozi tukiendelea na tabia ya  kupokea mapato bila kuangalia usalama wa watu sehemu ya kazi ni kweli kuwa tutapoteza wapiga kura wetu"


Masele alisema kuwa wizara yake inaendelea kutoa kutoa semina inayohusu uchimbaji katika mikoa yote Tanzania lengo ni kuwaelimisha wachimbaji huku akidai kuwa ukosefu wa elimu inachangia wachimbaji wengi kupoteza maisha


"Mfano eneo hili halifai kuchimba kwa kwenda chini kwa sababu ni sehemu ya udongo haina miamba kwa hiyo nirahisi kuporomoka na kufunika watu"alisema


Alitoa wito kwa wachimbaji kuzingatia usalama katika eneo la kazi,kuzingatia sheria za uchimbaji,kupokea utaalamu kwa wataalamu



MKUU WA MKOA ARUSHA


Akitoa salamu za pole mbele ya Waziri mkuu pamoja na viongozi wa dini,wananchi,wafiwa,viongozi mbalimbali Mkuu wa Mkoa Magessa Mulongo alisema kuwa tukio hilo ni kubwa sana huku akitoa shukrani kwa wananchi,vyombo mbalimbali vya dola kuwez kushirika katika zoezi la uokoaji miili


"Tukio lilitokea tarehe 1/4/saa 4 asubuhi na zoezi la uokoaji miili liliendelea hadi mida ya saa 12 jioni ambapo maiti 13 ziliokolewa



MEYA WA JIJI LA ARUSHA



Meya wa jiji hili Gaudence Lyimo alisema kuwa Taifa limepoteza vijana chapa kazi ambao ni  nguvu kazi  ya Taifa

Alisema uongozi wa jiji umeshiriki katika mchakato mzima wa maandalizi ya mazishi huku akitoa pongezi kwa jamii kujitolea kushiriki katika zoezi hilo lililokuwa gumu





KIONGOZI WA DINI



Mchungaji Kisiri Laizer wa kaninisa la kkkt dayosisi ya kaskazini kati aliwataka wafiwa kuwa na moyo wa uvumilivu na kuendelea kumuomba Mungu kwa kuwa yeye ndiye muweza wa yote



Hata hivyo wakati wa ziara hiyo viongozi mbalimbali waliweza kujionea hali halisi ya eneo hilo ambapo kifusi kingine kilidondoka katika eneo hilo mida ya saa 4 asbuhi ila  haikuleta madhara kwasababu hazikuwepo shughuli za uchimbaji



WALIOPOTEZA MAISHA MAJINA YAO


Nibart Raphael,Christipher L.Kawishe,Jerald Masai,Japheti Nellyang,Gerald Nellyang,Japhet Raphael,Elibariki Loseriani,Fabian Bambo,Fredy Loserian,Eliasi Fanuel,Alex Maliaki,Julius Peter Pallangyo,Gerald Jacob

No comments:

Post a Comment

 
Support : Katibu Mwenezi CCM (w) Arusha | Jasper Kishumbua | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali Blog - Arusha - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper Kishumbua
Proudly powered by Blogger